Tovuti hii ni mpya ambayo ni mahsusi kwa ajili ya kuwahubiria waliopotea injili isiyo ya bandia. Katika siku za usoni tutakuwa na masomo ambayo yatawajia hapa. Lakini kwa sasa, hebu niulize swali moja rahisi.Katika Mathayo 16:18, Yesu aliposema “juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu.” Ni mahali gani katika Agano Jipya alipoita kanisa “kanisa la Baptist”? Kama kanisa ni lake, sasa kwa nini kuliita kwa jina la tendo la wokovu? Tendo ambalo wabaptist wengi hawaamini kuanza nalo? Yesu alisema waziwazi ni “kanisa lake”. Ni dhahiri kwamba alilinunua kanisa kwa damu yake mwenyewe. Nasi tunaona majina ya kanisa katika Agano Jipya dhahiri shahiri. Walakini, hakuna mahali katika maandiko kwamba kanisa alilolinunua Kristo likaitwa Baptist. Hakuna. Kibiblia, mamlaka yako iko wapi ya kukufanya uliite kanisa alilolijenga Yesu, “Kanisa la Baptist”? Jina hili limetoka kwa Mungu au kwa mwanandamu? Na kama huwezi kupata mamlaka ya kibiblia ya jina la kanisa unalotumia. Je, hiyo haimaanishi kwamba basi tu huamini kwamba mamlaka ya Mungu imo katika Biblia?
Naomba ni nikuhabarishe kuhusu kanisa la Kristo. Hupatikana katika Afrika Mashariki, na ulimwenguni. Nao ni kundi la waamini, ambao sio tu wanajua kuwa Yesu alilijenga kanisa (Mathayo 16:18), Alilinua kwa damu yake mwenyewe (Mdo 20:28), bali pia ni kichwa cha kanisa (Wakol. 1:18). Hatuoni haya kuliita kanisa kwa jina la mwokozi wetu. Na wala hatuoni haya kuliita kanisa kwa jina lililoruhusiwa katika maandiko. Kwa nini Baptist wanakataa kujiita kwa jina la yeye aliyekufa kwa ajili ya kanisa lake?
Ndiyo kwanza natengeza hii tovuti kwa sasa na ni lazima nianzie mahali fulani. Vivile tunatoa masomo ya Biblia kwa masafa. Unaweza kutuma barua pepe kwenda kanisalakristo@yahoo.com ili kuomba masoma haya. Tafadhari usisahau kuandika jina na anwani yako ya posta.