Tafadhali Ukubali Kujulishwa Habari Ya Kanisa la Kristo

TAFADHALI UKUBALI KUJULISHWA HABARI YA KANISA LA KRISTO

Na Dale Dennis

Tunakujia wewe, katika jina la Kristo tu, tukiwa na hamu ya kukusaidia katika kutafta njia ya kweli ya uzima na tukitumaini kukusaidia katika kila jambo lililo haki.

Tunaamini kuwa Biblia ni andiko lenye pumzi ya Mungu ambalo linakamilisha watu na, kwa hiyo, Biblia PEKE YAKE ndiyo fundisho letu (2 Tim. 3:16-17).

Tunaomba kwa ajili ya umoja wa wote wanaomwamini Kristo kwa kuwa ndivyo alivyoomba Kristo Mwenyewe (Yoh. 17:20-21).  Paulo aliwasihi Wakristo wawe na “nia moja na shauri moja” (1 Kor. 1:10); akanena msingi wa pekee wa umoja katika Waefeso 4:1-6.

MAMBO MENGI YAKUPASAYO KUYAJUA

Inakupasa kujua kwamba:

Kanisa lilijengwa na kununuliwa na Yesu Kristo, Mat. 16:13-18; Mdo. 20:28.

Kanisa lilijengwa juu ya Yesu aliye msingi wa pekee, 1 Kor. 3:11.

Kanisa halikujengwa juu ya Paulo, wala Apolo, wala Kefa, wala mwingine awaye yote, 1 Kor. 1:12-13; 3:5.

Kanisa lilianzishwa, likasimamishwa imara katika siku ya Pentekoste ya kwanza baada ya kufufuka kwake Kristo aktika wafu, Lk. 24:49; Mdo. 1:8; Mk. 9:1; Mdo. 2:1-47.

Inakupasa kujua kwamba Kanisa si jengo au nyumba kama wanadamu wanayojenga, bali Kanisa ni watu:

Kol. 1:18; 1 Kor. 12:12-13, 27; 3:16; 1 Pet. 2:5; Mdo. 17:24.

Inakupasa kujua kwamba, katika Agano Jipya Kanisa limeitwa:

Hekalu la Mungu – 1 Kor. 3:16.

Mwili wa Kristo – Kol. 1:24; Efe. 1:22-23.

Ufalme wa Mwana wa Mungu – Kol. 1:13.

Nyumba ya Mungu – 1 Tim. 3:15.

Kanisa – Efe. 3:10.

Kanisa la Mungu – 1 Kor. 1:2; Mdo. 20:28.

Kanisa la Wazaliwa Wa Kwanza – Ebr. 12:23.

Makanisa ya Kristo – Rum. 16:16.

Inakupasa kujua kwamba watu ambao wamezidishwa katika Kanisa na Bwana huitwa:

Viungo vya mwili wa Kristo – 1 Kor. 12:27.

Wanafunzi – Mdo. 6:1.

Walioamini – Mdo. 5:14.

Watakatifu – Mdo. 9:13.

Makuhani, Ukuhani – Ufu. 1:6; 1 Pet. 2:9.

Wana wa Mungu – 1 Yoh. 3:1-2.

Wakristo – Mdo. 11:26, 28; 1 Pet. 4:16.

Inakupasa kujua kwamba katika Kansia kuna:

Wazee ambao wote ni maaskofu (Tito 1:5-9) na waangalizi (Mdo. 20:17-18, 28) na wachungaji (1 Pet. 5:1-4).  Si kana kwamba tumetaja aina nne za watu wenye kazi mbalimbali, la sivyo!  Sura hizo zinatuaonyesha wazi kwamba kila mzee wa kanisa ni askofu, na mwangalizi na mchungaji pia; kwa kuwa, kazi yake ni kuangali, na kuchunga, na kutunza na kulisha kanisa.  Mtu hawezi kuwa mzee wa kanisa isipokuwa ametimiza yote yaliyoandikwa katika 1 Tim. 3:1-7 na Tito 1:5-9.

Katika kansia kuna mashemasi.  Kazi yao ni kulihudumia kanisa, 1 Tim. 3:8-13;  Mdo. 6:1-6.

Katika kanisa kuna kuhani mkuu.  Yesu Kristo ni kuhani mkuu wetu na hakuna mwanadamu awaye yote awezaye kuwa kuhani mkuu pamoja na Kristo, Ebr. 4:14; 7:23, 24, 28; 7:11, 12; Rum. 6:14; Gal. 3:23-26.

Katika kanisa kuna makuhani, KILA MKRISTO ni kuhani (Ufu. 1:6; 1 Pet. 2:9) na kazi ya kila Mkristo ni kujitoa mwili wake uwe “Dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu,” Rum. 12:1, na kumpa “dhabihu ya sifa daima, yaani, tunda la midomo iliyoungama jina lake,” na sadaka ya “kutenda mema na kushirikiana” Ebr. 10:12-14; 9, 12.  Lakini, tunapokula chakula cha Bwana, si kana kwamba tunamtoa Kristo awe dhabihu tena; bali chakula cha Bwana ni ukumbushao tu wa kifo chake (1 Kor. 11:23-26).

Inakupasa kujua kwamba mwanadamu:

Hakukusudia kanisa, bali Mungu alikusudia, Efe. 3:10-11.

Mwanadamu hakununua kanisa, bali Yesu alinunua, Mdo. 20:28; Efe. 5:25.

Mwanadamu hakuwapa watu wa kanisa jina lao, bali Mungu aliwapa jina, Isa. 62:2; Mdo. 11:26.

Mwanadamu hakuliita kansia kuwa ni mali yake, bali Yesu aliliita kanisa kuwa ni lake, Mat. 16:18.

Mwanadamu si kichwa cha kanisa, bali Yesu ni kichwa cha kanisa, Efe. 5:23; 4:4; 1:22, 23.

Mwanadamu si mwokozi wa kanisa, bali Yesu ni mwokozi wake, Efe. 5:23.

Mwanadamu hakulipa kanisa mafundisho yake, bali Yesu alilipa mafundisho yake, Gal. 1:11; 2 Pet. 1:20-21; 2 Yoh. 9-11.

Mwanadamu hakulizidisha kanisa, bali Yesu alizidisha kansia kwa wale waliokolewa, Mdo. 2:47.

Inakupasa kujua kwamba kanisa na mwili wa Kristo ni mamoja:

Efe. 1:22-233; Kol. 1:18, 24.

Inakupasa kujua kwamba Agano Jipya linasema:

Kuna ufalme mmoja wa Kristo, Kol. 1:13-14.

Linasema kuna mwili mmoja wa Kristo, Efe. 1:22-23; 4:4.

Linasema kuna kansia moja tu la Krsito, Mat. 16:18; Efe. 1:22-23; 4:4; Yoh. 17:20-21.

Inakupasa kujua kwamba katika Kanisa tu tunaweza kupata:

Ukombozi, Efe. 1:7.

Msamaha wa dhambi katika kanisa tu, Kol. 1:13-14.

Kutakaswa katika kansia tu, Efe. 5:26.

Baraka zote za rohoni katika kansia tu, Efe. 1:3.

Inakupasa kujua kwamba ili uingie katika Kanisa ni lazima:

Kumwamini Kristo, Yoh. 8:24; Mdo. 16:31; Ebr. 11:6.

Ni lazima kuzitubia dhambi, Lk. 13:3; Mdo. 2:38; 3:19; 17:30.

Ni lazima kukiri imani yako katika Kristo, Mat. 10:32-33; Rum. 10:10; Mdo. 8:37-38.

Ni lazima kubatizwa, Mat. 28:19; Marko 16:16; Mdo. 2:38; 10:48; 22:16; 1 Pet. 3:21; Gal. 3:27.

Inakupasa kujua kwamba ubatizo:

Huhitaji maji, Mdo. 10:47.

Ubatizo huhitaji maji mengi, Yoh. 3:23.

Ubatizo huwafanya watu waende mahali penye maji, Mdo. 8:36; Mat. 3:5, 6;  Yoh. 3:23.

Ubatizo huwafanya watu waingie ndani ya maji, Mdo. 8:38.

Ubatizo humfanya mtu kuzikwa ndani ya maji, Rum. 6:3-5; Kol. 2:12.

Ubatizo humfanya mtu kuzaliwa tena, Yoh. 3:5.

Ubatizo humfanya mtu kufufuka kutoka maji, Kol. 2:12.

Ubatizo huwafanya watu kupanda kutoka maji, Mdo. 8:39; Mat. 3:16.

Inakupasa kujua kwamba katika ubatizo:

Dhambi huoshwa, Mdo. 22:16.

Twaokolewa kutoka dhambini, 1 Pet. 3:21; Mk. 16:16.

Twapata ondoleo la dhambi, Mdo. 2:38.

Twaingia katika Kristo na twamvaa Kristo, Gal. 3:27.

Twaokolewa kutoka hukumu ya adhabu, Gal. 3:27; Rum. 8:1.

Twaingia katika kanisa, Mdo. 2:27-47.

Twaanza kutembea katika upya wa uzima, Rum. 6:3-5.

Twamtii Kristo, Mdo. 10:48; Mk. 16:16.

Twapokea kipawa cha Roho Mtakatifu, Mdo. 2:38; 5:32.

Inakupasa kujua kwamba ni lazima kuwa kanisa kumwabudu Mungu:

Katika roho na kweli, Yoh. 4:23-24; Rum. 12:1.

Twaabudu KILA SIKU bila kukoma, kwa njia ya kutoa miili yetu iwe “Dhabihu iliyo hai.”  Rum. 12:1.

Twaabudu katika kila neno na kila tendo, Kol. 3:17, 23, 24.

Twaabudu katika matendo mema, Efe. 2:10; Mat. 5:16; Ebr. 13:16; Mat. 25:31-46.

Twaabudu katika kuliungama jina lake Yesu “daima”, Ebr. 13:15; Mat. 10:32-33.  Hii ina maanda ya kuwa ni lazima kwa kila Mkristo kumkiri Yesu na kuifundisha Injili yake kwa watu wengine, Ebr. 5:12; Mat. 28:18-20; 1 Pet. 3:15.

Twabudu katika kuomba, Mdo. 2:42; 1 Tim. 2:1-2.

Twaabudu katika kuimba, Efe. 5:19; Kol. 3:16.

Twaabudu katika kujengana, 1 Kor. 14:26-27.

Twaabudu kwa kula chakula cha Bwana katika Siku ya Kwanza ya juma, Mdo. 20:7; 1 Kor.11:23-32; Ebr. 10:26.

Twaabudu katika kutoa changizo, 1 Kor. 16:1-2; 2 Kor. 8:1-15; 9:1-15; Mdo. 20:35.

Twaabudu kwa kudumu katika kujifunza maneno ya Mungu, Ebr. 5:12-14; 1 Pet. 2:2; Mat. 4:4.

Inakupasa kujua kwamba kazi ya kila Mkristo ni:

Kuihubiri Injili, Mk. 16:15; Mat. 28:18-20; 1 Tim. 4:1-7.

Kila Mkristo na afundishe wengine, Ebr. 5:12; 1 Pet. 2:9; 3:15; Efe. 3:10-11.

Wakristo wote wapendane na kufanya matendo mema, 1 Yoh. 3:11-18; Mat. 25:31-46; Ebr. 13:15; Efe. 2:20; Yak. 1:27; Rum. 12:1-2.

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Twitter picture

You are commenting using your Twitter account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s