“Sheria yako naipenda mno ajabu, ndiyo kutafakari kwangu mchana na usiku. Kufafanusha maneno yako kwatia nuru, na kumfahamisha mjinga” Zaburi 119:97, 130
Wakristo walio wengi wanatambua jinsi Mungu alivyofanya kazi kwa takribani miaka 1,500, na waandishi 40 tofauti tofauti ili kutupa Neno lake takatifu. Neno lililotolewa ili kufunua mapenzi ya Mungu kwa wanadamu (Yohana 5:28:11-13). Nasi vivyo hivyo tunatambua kwamba tukishabatizwa, ni lazima tufundishwe kuyashika yote, Mathayo 28:20. Tunatakiwa kuyatamani maziwa yasiyoghoshiwa ya Neno la Mungu, Petro 2:2. tulishike lililo jema, 1 Wathesalonike 5:21. Kulitumia kwa halali neno la kweli, 2 Timotheo 2:15. Tuachane na maziwa na tuufikie utimilifu, Waebrania 6:1, wakati huo huo tunaendelea kuwafundisha wengine kuyashika tuliyojifunza., 2 Timotheo 2:2.
Tumebarikiwa mno kuwa na maneno haya yakiwa yameandikwa kwenye kurasa, 2 Timotheo 3:16-17. Maneno ambayo kwayo twaweza kujifunza hasa Mungu anachotaka tujue, kufanya na kutii ili tuwekwe huru, Yohana 8:32; Waebrania 5:9.
Licha ya kuwa na ukwasi kama huu duniani, ni fedheha bado ipo njaa ya kulazimisha au ya kujitakia. Sio njaa ya ngano au mkate, bali njaa ya neno la Mungu kama vile alivyotangaza nabii Amosi, Amosi 8:11. Na sio kwamba maneno ya Mungu hayapo, ni kwamba leo wengi wamejisababishia njaa ya kiroho maishani na majumbani mwao kwa visingizio, kuridhika, ajizi, uvivu, n.k. licha ya kuificha injili kwa waliopotea (2 Wakorintho 4:3); twafanya vema kujificha injili.
Yaweza kusemwaje juu ya wale ambao hawasomi tena neno la Mungu? Tayari wanafahamu kuwa ni kitabu bora kupata kuandikwa.Ndani yake kuna hadithi ya upendo iliyopata kusimuliwa. Na jinsi ambavyo ndani yake yamo maneno yaongozayo kwenda kwenye uzima wa milele. Bado kwa wengi, kiwango fulani cha kumfahamu Kristo na kanisa kinatosha kuwafurahisha. shauku na ghamu ambayo wanapaswa kuwa nayo, ilishatoweka zamani.
Nataka tuangalie kwa haraka Mathayo 22:29-32. Twaweza kuona hapa Yesu na Masadukayo walikuwa wanazungumizia juu uhalisia wa ufufuo. “Yesu akajibu akawaambia, Mwapotea kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu,” Mathayo 22:29. Maana ya Yesu ni dhahiri, Masadukayo walishikilia imani potofu juu ya fundisho hili, kwa sababu walishindwa kuyasoma maandiko. Jibu lilikuwepo, na walichotakiwa kufanya ni kusoma na kujionea wenyewe. Bado hawakuweza kwa sababu fulani fulani.
Kuna namna kadha wa kadha inayoweza kutumika kuwianisha mistari hii na hali ya leo. Ninachotaka tujikite nacho ni kwamba tunatakiwa kujifunza kwamba Mungu “ametukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa,” 2 Petro 1:3. Na kama tukikataa kujifunza maandiko, na kuijua kweli kuhusiana na mafundisho fulani, ndipo tunakuwa na hatia kama Masadukayo vile vile, kama Yesu alivyosema, “Mwapotea.”
Unaweza kudhani kuwa, kwa hiyo “napotea” kidogo kwa kutojua fundisho la Kristo kama inipasavyo. Na upungufu huu wa ufahamu unaweza usikunyime usingizi. Walakini ilipasa ukunyime usingizi. Maana, katika Mathayo 22:29 Yesu aliposema “mwapotea kwa kuwa hamyajui maandiko.” Yesu aliwajulisha Masadukayo kuwa huu “haukuwa ufinyu wa uelewa.” Huu ni ukosefu unaoumiza ambapo wautendao watahukumiwa kwa huo.”
Tuzingatie kuwa utohoaji wa neno “kosea” katika Kiyunani ni “planao,” neno ambalo limetokana na neno la Kiyunani “plane.” Humaanisha “sababisha kukosea, tangatanga, potea,potosha, hangaika na kuwa nje ya njia.” Hivyo, hapa tunaona Yesu alivyowachukulia ambao hawakuyajua maandiko kama iwapasavyo, ingawaje walikuwa na fursa kufanya hivyo. Walikuwa wanapotea tu!
Bado hata sasa ningali sifahamu endapo kuna watu watakaokuwa wanafahamu nguvu ya maneno “Planao” na “plane.” Labda tukiangalia mahali pengine ambapo maneno hayo yametumika inaweza kutusaidia kuelewa kiuhalisia jinsi alivyowachukulia walioshindwa kupenda na kujua maandiko kama walivyopaswa. Hebu tuone aya mbili:
- 2 Wathessalonike 2:3, 11 Mtu yeyote asiwadanganye kwa njia yoyote; maana haiji, usipokuja kwanza ule ukengeufu; akafunuliwa yule mtu wa kuasi, mwana wa uharibifu; Kwa hiyo Mungu awaletea nguvu ya upotevu, wauamini uongo;
- Neno “nguvu” katika mstari wa 11 limetokana na neno “plane” ambalo tumetoka kuliona. Ona katika mstari wa 3, Paulo aliwaonya ya kwamba mtu yeyote asiwadanganye. Na katika mstari wa 10, Paulo anabainisha kwamba wale wasioipenda kweli ndipo katika mstari wa 11, wataletewa nguvu (plane), na watauamini uongo kabisa. Na madhara ya kuuamini uongo huu yapo katika mstari wa 12, HUKUMU!
- Warumi 1:27-wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyowapasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao.Unajua neno “potea” liko kwenye kiyunani? Uko sahihi, kama lililopo hapo juu, “plane.”
Hivyo, twaweza kuona matumizi ya aina mbili ya neno lile lile alilolitumia Yesu alipowashutumu Masadukayo kwa kutojua maandiko kama walivyopaswa. Matumizi ya kwanza huonyesha kuamini mafundisho ya uongo, ambapo huleteleza hukumu ya adhabu. Na matumizi ya pili huhusisha ushoga, ambapo pia hupelekea hukumu ya adhabu.
Tuzisome Biblia zetu kama itupasavyo! Tusibweteke na machache tunayoyafahamu! Bali kama vile kurungu avalishwavyo kwa maji, nasi tuyavae Maneno ya ajabu ya Uzima!